WARUMI7

Hatufungwi Tena Na Sheria

1 Ndugu zangu (sasa ninasema na wale wanaoijua sheria), je, hamjui ya kwamba sheria ina mamlaka tu juu ya mtu wakati akiwa hai? 2
Kwa mfano, mwanamke aliyeolewa amefungwa kwa mumewe wakati akiwa hai,
lakini yule mume akifa, yule mwanamke amefunguliwa kutoka sheria ya
ndoa.
3
Hivyo basi, kama huyo mwanamke ataolewa na mwanaume mwingine wakati
mumewe akiwa bado yuko hai, ataitwa mzinzi. Lakini kama mumewe akifa,
mwanamke huyo hafungwi tena na sheria ya ndoa, naye akiolewa na mtu
mwingine haitwi mzinzi.

4
Vivyo hivyo, ndugu zangu, ninyi mmeifia sheria kwa njia ya mwili wa
Kristo, ili mweze kuwa mali ya mwingine, yeye ambaye alifufuliwa kutoka
kwa wafu, ili tupate kuzaa matunda kwa Mungu.
5
Kwa maana tulipokuwa tunatawaliwa na asili ya dhambi, tamaa za dhambi
zilizochochewa na sheria zilikuwa zikitenda kazi katika miili yetu,
hivyo tulizaa matunda ya mauti.
6
Lakini sasa, kwa kufia kile kilichokuwa kimetufunga kwanza, tumewekwa
huru kutokana na sheria ili tutumike katika njia mpya ya Roho, wala si
katika njia ya zamani ya sheria iliyoandikwa.

Sheria Na Dhambi

7
Tuseme nini basi? Kwamba sheria ni dhambi? La, hasha! Lakini,
isingekuwa kwa sababu ya sheria, nisingalijua dhambi. Nisingalijua
kutamani ni nini kama sheria haikusema, “Usitamani.”
8
Lakini dhambi kwa kupata nafasi katika amri, hii ikazaa ndani yangu
kila aina ya tamaa. Kwa maana pasipo sheria, dhambi imekufa.
9Wakati fulani nilikuwa hai pasipo sheria, lakini amri ilipokuja, dhambi ikawa hai, nami nikafa. 10 Nikaona kwamba ile amri iliyokusudiwa kuleta uzima, ilileta mauti. 11 Kwa maana dhambi kwa kupata nafasi katika amri, ilinidanganya, na kupitia katika hiyo amri, ikaniua. 12 Hivyo basi, sheria yenyewe ni takatifu, na amri ni takatifu na ya haki, tena ni njema.

13
Je, kile kilicho chema basi kilikuwa mauti kwangu? La, hasha! Lakini
ili dhambi itambuliwe kuwa ni dhambi, ilileta mauti ndani yangu kupitia
kile kilichokuwa chema, ili kwa njia ya amri dhambi izidi kuwa mbaya
kupita kiasi.

Mgongano Wa Ndani

14 Kwa maana tunajua kwamba sheria ni ya kiroho, lakini mimi ni wa kimwili nikiwa nimeuzwa kwenye utumwa wa dhambi. 15 Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia. 16 Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, ni kwamba ninakubali kuwa sheria ni njema. 17 Lakini, kwa kweli si mimi tena nitendaye lile nisilotaka bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 18
Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna jema lolote likaalo ndani yangu,
yaani, katika asili yangu ya dhambi. Kwa kuwa nina shauku ya kutenda
lililo jema, lakini siwezi kulitenda.
19 Sitendi lile jema nitakalo kutenda, bali lile baya nisilolitaka, ndilo nitendalo. 20 Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.

21 Hivyo naiona sheria ikitenda kazi. Ninapotaka kutenda jema, jambo baya liko papo hapo. 22 Kwa maana katika utu wangu wa ndani naifurahia sheria ya Mungu. 23
Lakini ninaona kuna sheria nyingine inayotenda kazi katika viungo vya
mwili wangu inayopigana vita dhidi ya ile sheria ya akili yangu. Sheria
hii inanifanya mateka wa ile sheria ya dhambi inayofanya kazi katika
viungo vya mwili wangu.

24 Ole wangu mimi maskini! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?

25Ashukuriwe
Mungu kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu! Hivyo basi, mimi mwenyewe kwa
akili zangu ni mtumwa wa sheria ya Mungu, lakini katika asili ya dhambi
ni mtumwa wa sheria ya dhambi.

JIBU MASWALI.

 QUIZ